Kimsingi kanuni ya ufanyaji mapenzi iko zaidi kwenye ubongo kuliko mwilini. Kinachotokea hadi mtu akapata msisimko wa kufanya mapenzi si mwitikio wa mwili, bali ni utambuzi wa akili juu ya kiwango cha mwanamke anayefaa kimapenzi.
Katika hali ya kawaida nguvu ya kupenda inayomwingia mtu huwa kubwa, lakini suala la kupunguza ukubwa wa hisia lazima lipewe kipaumbele. Jambo kubwa linalowasumbua wanaume wengi wenye tatizo la kufika kileleni mapema ni kuwa na PUPA ya kufanya ngono.
Anachotakiwa kufanya ni kutumia zaidi ya dakika 20 kufanya maadalizi na mpenzi wake kabla ya kuanza tendo. Hii itasaidia kuufanya mhemko wake ushuke na kumuongezea muda wa kumaliza.
Mume na mke wanapoingia katika uwanja wa mapenzi wakae kwanza kwa muda, huku wakiwa wamejiachia na mavazi mepesi. Pili wacheze michezo mingi kwa muda mrefu bila kuanza kazi yao. Wakiwa kwenye hamasa hizo wasiwe kimya bali wazungumze na kuulizana maswali ya kimahaba.
Baada ya hapo mbinu nyingine ya kuzuia mbegu za kiume zisitoke ni ile ya kujibana. Inashauriwa kuwa mwanaume akiona dalili za awali za kumaliza bila kujali ametumia muda gani anachotakiwa kufanya ni kukaza misuli ya miguu na kuzuia mbegu kwa mtindo atumiao kuzuia haja ndogo isitoke.
Kujibana huko kunatakiwa kuende sambamba na kuacha kucheza �shoo�. Pacha na hilo mwanaume anatakiwa kuidanganya akili kwa kuilazimisha iwaze jambo jingine hasa la kuhuzunisha ili kuharibu taarifa za raha zilizotumwa mwilini zisiendelee kufanyiwa kazi na hatimaye kumaliza tendo haraka.
Zoezi hili linaweza kuwa gumu katika hatua za kwanza kutokana na kukosea muda sahihi wa kujizuia, lakini mhusika akiendelea kujizoeza atajikuta anaweza na kupata uwezo wa kufanya mapenzi hata kwa saa nzima, hivyo kuondokana na tatizo hilo bila tiba wala madhara.
http://studentswagas.blogspot.com/
 
Top